SHEHA MADUNGU AIOMBA SERIKALI KULIPATIA UFUMBUZI SUALA HILI KUNUSURU WATOTO KUJIINGIZA TENA KATIKA TABIA HATARISHI

           

NA AMINA AHMED MOH’D - PEMBA. 

SHEHA  wa Madungu, eneo liliopo katikati ya mji wa Chake Chake,Pemba,  ameitaka serikali  kuangalia  vyema utowaji  vibali  vya kuendesha   michezo  ya  video ili kudhibiti   kuporomoka kwa maadili  na tabia za watoto. 

        

 MAFUNDA HAMAD RUBEA - SHEHA MADUNGU  

 Aliishauri serikali kuweka masharti maalum  ya uendeshaji wa biashara hiyo na kufuatiliwa utekelezaji wake.

Katika mahojiano maalum, Sheha wa Madungu,  Mafunda Hamad Rubea alisema juhudi za kuondoa athari za michezo hio kwa watoto zinazochukuliwa na uongozi kwa kushirikiana na wananchi  wa shehia hiyo bado hazipata ufanisi mkubwa.

Alisema wamiliki bado hawajakubali kufunga biashara hiyo kwa madai wanatambulika kisheria kama walipa kodi, lakini ukweli ni kwamba biashara hii inachangia kuharibika kwa watoto kimaadili na kufanyiwa vitendo viovu  . 

‘’Tunashirikiana na wananchi kuipiga marufuku michezo hii,  lakini bado wamiliki wanadai wanafanya kihalali kwa vile wamepewa vibali vya kufanya biashara hii. Kwahivyo, nguvu yetu imekuwa ndogo na tunaiomba serikali iipige marufuku michezzo hii nchi nzima’’, aliongeza. 

 Alisema michezo hii imepeleka  watoto kurubuniwa na kudhalilishwa ili wapate pesa zitazowawezesha kwenda   kucheza video.

Bi Mafunda aliwtaka wazazi  na walezi kuendelea kushirikiana katika kudhibiti maadili ya watoto na vijana ,ikiwa ni pamoja na kufuatilia mienendo ya watoto ili kuwaepusha kujiingiza katika vitendo viovu vinavyoweza kuwaharibia maisha. 

Alisema endapo wazazi wataendelea kumuunga mkono katika  kudhibiti michezo hatarishi ikiwemo  kama hii ya video, mikusanyiko katika maskani za vijana na uzururaji hovyo mitaani  watakutasaidia  kudhibiti  maadili kwa watoto katika shehia hiyo.

" Wazazi na walezi watoe mashirikiano  katika kuendeleza tabia njema kwa watoto na vijana kwani bado vipo viashiria katika baadhi ya mitaa na kwa bahati mbaya baadhi ya wazazi hawatoi mashirikiano mazuri ni vyema kushirikianakwa pamoja katika kujenga taifa la baadae ",alisema.

 Baadhi ya wananchi  katika shehia hiyo, wakiwemo Abdulahman  Muhamed na Jamila Muhamed, walisema juhudi za kudhibiti maadili na kuondoa vitendo viovu zinazofanywa na sheha huyo  zinahitaji msaada wa ngazi za juu  za serikali

Hii ni pamoja na  kutoa maamuzi juu ya kudhibiti  na kuondoa hii michezo mitaani. 

 "Wapo wazazi ndani ya hii shehia wanaotia pamba masikioni juu ya hili, lakini tupo tunaomuunga mkono sheha na mafanikio yameanza kuonekana. Mengine yaliobaki ni  serikali kweka nguvu zaidi" Alisema Abdulrahman. 

"Baadhi ya wananchi tumekuwa wagumu kutoa mashirikiano, jambo ambalo linalrudisha nyuma jitihada za shehia kudhibiti  maadili ipasavyo. Bado hatujashikamana kwani wakati  tumejikubalisha kujenga wengine wanabomoa   kimya kimya’’, alisema Bi.Jamila. 

 Katika kudhibiti maadili kwa vijana na watoto ndani ya shehia  ya Madungu   uongozi pia unawashirikisha viongozi wa dini  na  waalimu wa skuli na  madrasa.

Mitaa inayoogoza kwa michezo hii inayoaribu mwenendo wa watoto katika sheha hio ni Madungu, Fueni na Mtoni. 

 Mwisho.

 

 



 

 






 

 


Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI