MAMLAKA YA MAPATO ZANZIBAR ( ZRA) YAWATOA HOFU WANANCHI JUU YA KODI YA MAJENGO ZANZIBAR.

NA AMINA AHMED MOH’D PEMBA. 

MAMLAKA  ya mapato Zanzibar ( ZRA ) Imewatoa hofu wananchi kuhusu maneno ya upotoshaji yanayoendelea kutolewa   na baadhi ya wananchi wasiopenda maendeleo  juu ya  ukusanayaji wa kodi ya majengo  ambapo imesema kodi hiyo haitowahusu  wamiliki wa nyumba za kawaida za makazi  kama inavyosambazwa na baadhi  ya watu wachache wasio na uelewa. 

 Akizungumza na viongozi wa mkoa kusini na kaskazini Pemba Kamshina mkuu wa mamlaka hiyo Zanzibar  Yussuf Juma Mwenda amesema kuwa  majengo ya ghorofa  yanayofanyiwa biashara  pekee ndio ambayo yatahusika na kodi hiyo  ambayo  pia haitowaumiza wamiliki wake  kutokana na unafuu uliowekwa. 

"Mitaani kuna maneno uko lakini ukweli haupo ivyo unavyosemwa  mitaani, ukweli ni kuwa kodi hii sio ya wote bali ni ya watu wachache ambao wanamiliki majengo ya ghorofa". 

 Na wao pia haitowaumiza hiyo kodi kwa sababu ni yenye unafuu  mno ni kodi ambayo kwa mwaka  kila mmiliki atalazimika kulipa shilingi 10000 tu ambayo kwa mwezi ni sawa na shilingi 830 lengo ni kuongeza makusanyo kupitia vyanzo mbali mbali kwalengo la kuleta maendeleo ". Alisema. 

 Aidha Mwenda amesema kuwa Serikali ya Zanzibar inayoongozwa na Dk Hussein Ali Mwinyi  katika kuhakikisha inarahisisha maisha bora kwa wananchi wake imeamua  kutokuziingiza nyumba za kawaida katika kodi ya majengo kama zilivyo katika nchi nyengine. 

 "Mh Rais Katika kuwajali wananchi wake ametutaka  nyumba za kawaida za wananchi tusiziweke katika kodi hii ya majengo, akatutaka pia  hizo kodi katika hayo majengo zisiwaumize wananchi  hakuna popote ambapo jengo linalipiwa gharama hiyo kwa mwezi isipokuwa Zanzibar ". 

Aidha kamishna  amewataka viongozi wa  shehia wilaya na mikoa kuwasaidia kuyatambua majengo  hayo pamoja na wamiliki wake ambayo yamo katika shehia zao sambamba na kutoa elimu sahihi kwa wananchi juu ya ulipaji  kodi ya majengo. 


 Akizungumza katika mkutano huo  Mkurugenzi ZRA Pemba Jamal Hassan Jamal amesema lengo la kurudishwa upya kodi hiyo  ni katika kuleta maendeleo kwa wananchi ikiwemo kuboresha miundo mbinu afya  pamoja na  elimu ambao kodi hizo zinazokusanywa na mamlaka hiyo  hutumika kwa matumizi mbali mbali ya wananchi. 

Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika mikutano hiyo mkuu wa mkoa wa Kaskazini   na Kusini Pemba Salama Mbarouk Khatib Pamoja na Mattar Zahor Massoud  wamesema   wataendelea kuiunga mkono serikali katika kushajihisha  zaidi ukusanyaji wa kodi mbali mbali ili kuweza kupanga zaidi  mipango ya maendeleo. 

 Kodi ya majengo Zanzibar imeanzishwa kwa mujibu wa Sheria namba 14  mwaka 2008 lengo ikiwa ni kuongeza vyanzo vya mapato ya kukusanya kodi Zanzibar Ambapo mikutano hiyo maalum iliyoandaliwa na mamlaka hiyo katika ukumbi wa Baraza la wawakilishi Wete Upande wa kaskazini sambamba na  Baraza la Manispaa Chake Chake ambao viongozi wa shehia na viongozi mbali mbali walishiriki katika mkutano huo. 

 




.
 

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI