MAGANYA AWATAKA VIONGOZI WA CCM KUSINI KUSIKILIZA CHANGAMOTO ZA WANANCHI NA KUZIPATIA UFUMBUZI

NA AMINA AHMED MOH’D. 

WANA chama wa chama  cha Mapinduzi mkoa wa  kusini Pemba   wamempokea kwa vifijo na nderemo  mlezi mpya wa  Chama hicho  mikoa miwili ya Pemba Fadhil Rajab Maganya  aliewasili kisiwani humo kwa ziara maalum ya kujitambulisha   ikiwa ni mara ya kwanza  tokea  kutangazwa kushika nafasi  hiyo.
         FADHIL RAJAB MAGANYA - MLEZI CCM MIKOA MIWILI YA PEMBA. 

Akiungumza kwa nyakati tofauti  na wanachama wa chama cha Mapinduzi  wilaya ya  Mkoani pamoja na  Chake chake  mlezi huyo amewataka  kuendeleza mashirikiano   katika kuimarisha chama na jumuia zake ikiwa ni pamoja na kubuni miradi mbali mbali ya maendeleo. 

Amesema  mashirikiano kati ya wanachama na viongozi ikiwemo kutatua changamoto , kutekeleza ilani ya chama ndio nyenzo pekee itakayosaidia  kuleta maendeleo kwa wananchi.  

" Kamati za siasa mkoa wa kusuni Pemba naomba mashirikiano ambayo kwa pamoja  yatawaweka karibu na wanachama  pamoja na wananchi kwa kusikilza changamoto  na kuzipatia ufumbuzi  kero  na changamoto zao". 

"Kukwepa kwepa  kutokuwa na mashirikiano  ni chanzo cha migogoro na mimi kitu ambacho sikihitaji ni kutatua mgogoro  ninanchohitaji ni kuona mafanikio na maendeleo ya kukiimarisha chama ili kupata ushindi  2025".

 Aidha mlezi huyo  ameupongeza uongozi wa chama hicho  Mkoa wa kusini Pemba kwa Mashirikiano mazuri aliyoyapata ambapo amesema kuwa hiyo ni  ishara njema ya  ya maendeleo kwa Serikali inayosimamiwa na chama cha Mapinduzi. 

 Aidha Maganya amesema kuwa   ataendelea kuitumikia vyema nafasi hiyo ililengo lililokusudiwa la kuimaraisha na kuongeza nguvu katika  chama hicho  liweze kufikiwa.

 Awali akitoa salam za  chama  mwenyekiti wa CCM mkoa huo  Yussuf Ali Juma ameahidi mashirikiano  kwa mlezi huyo  ambapo amesema uongozi na wanachama utaendelea kusimamia na kutekeleza maagizo yote yaliotolewa  yenye lengo ya kukisogeza mbele zaidi chama hicho
 Nae kwa Upande wake Katibu wa chama hicho mkoa huo  Ramadhan Hassan Rajab amemshukuru  mlezi huyo kwa kufanya  ziara hoyo  maalum ndaninya mkoa huo   ambapo wamesema chama na jumuia zake kitaendelea kumuunga mkono katika kusimamia majukumu aliyokabdihiwa. 

Ziara hiyo licha ya kutembelea na kuzungumza  wanachama wa wilaya mbili zilizomo ndani ya mkoa huo  lakini pia mlezi huyo alitembelea na kukagua ujenzi wa milango ya  maduka ya chama   cha Mapinduzi iliyopo  Chachani, Gombani pamoja na kutembelea kaburi la  Aliekuwa Makamu wa rais wa Jamuhuri ya Muungano Tanzania Dk Omar Ali Juma Wawi pamoja na kumuombea dua ambapo ziara hiyo ya siku mbili kusini  imefikia tamati na kuelekea Kaskazini  pemba kwajili ya shughuli hiyo ya kujitambulisha. 


Mwisho. 


Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI