KATIBU MKUU WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI ZANZIBAR ATETA NA WANAFUNZI KOJANI.

NA AMINA AHMED MOH’D, PEMBA. 

WANAFUNZI  wa Skuli za Sekondari kisiwani Pemba  wametakiwa kuthamini juhudi zinazofanywa na serikali katika kurahisisha upatikanaji wa huduma bora za elimu katika skuli mbali mbali  ikiwa ni pamoja na kutumia huduma za maktaba kujisomea vitabu mbali mbali vilivyotolewa .


 Ametoa ushauri huo katibu mkuu wizara ya elimu na mafunzo ya amali  Zanzibar Khamis Abdalla Said  Alipokuwa akizungumza  na wanafunzi wa madarasa ya Sekondari Kojani Mkoa wa Kaskazini Pemba  alipofika  kisiwani humo na kufanya ziara ya kustukiza kuangalia  maendeleo ya wanafunzi mapema leo asubuhi.

 Amesema licha ya serikali kuendelea kuboresha na kuweka mazingira rafiki  kwa wanafunzi  lakini bado wanafunzi wamekuwa wakikosa kuzithamini juhudi hizo  na kupelekea kupatikana ufaulu usioridhisha kutokana na kushindwa kuzitumia fursa hizo za kujisomea vitabu  vya masomo mbali mbali.

 "Serikali imekuwa ikijitahidi kuboresha mazingira ya elimu katika skuli zote, kuboresha majengo kuweka vifaa, vya kufundishia ambavyo ni vya kisasa  vitabu  waalimu lakini bado utumiaji wa maktaba (Library)  umekuwa hauridhishi  wanafunzi hawaoni  iyo fursa . "

" Niwaase wanangu mthamini jitihada zinazofanywa na serikali  kwajili ya kuwaandalia maisha bora baadae mzitumie maktaba hizi zilizopo skuli msome vitabu mpate kuongeza ufahamu   msiziwache zikaingiwa na vumbi ".

 Aidha  katibu huyo amewataka  wanafunzi  wanaotarajia kufanya mitihani ya kidato cha nne   kisiwani humo kuongeza bidii katika masomo ili waweze kupata matokeo mazuri  yatakayobadilisha maisha yao na kuzifikia fursa mbali mbali.

Akizungumza Kwa upande wake mwalimu mkuu skuli ya Sekondari Kojani  Khamis Amour Khamis ameushukuru uongozi huo uliofika katika  skuli hiyo kwa nia ya kutaka kujionea maendeleo ambapo amesema itasaidia kuwa chachu  ya mabadiliko kwa wanafunzi katika kuongeza kasi zaidi ya masomo yao. 

"Yeye kafanya ziara kutushtukiza lakini hii kwetu sisi ni faraja kuona kuwa kiongozi  anajali suala la elimu itasaodia kuongeza hamasa  kwa vijana kusoma. 

  Nao baadhi ya Wanafunzi  wamesema matarajio yao ni kupata ufaulu mzuri katika masomo ya sayansi ili  kuweza kuwa wataalamu wazuri baadae. 

 Mwisho. 

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI