VIJANA WATEMA CHECHE SERA ZINAZOBADILIKA BADILIKA Habari

Na Amina Ahmed Moh’d Pemba. 

ZAIDI ya Vijana 40 Kutoka  maeneo na Taasisi mbali mbali  Kusini na Kaskazini   mwa kisiwa cha  Pemba  Leo hii Wameshiriki katika Kongamano Maalum  la kujadili Masuala ya kidemocrasia  na ushirikishwaji  wa Vijana katika Siasa, Democrsia,  Jamii na Uchumi, Yalioandaliwa na   Kijana High Faundation, Taasisi ya Youth Initiative,   Pamoja na Taasisi ya   One Young Tanzania lililofanyika katika ukumbi wa Makonyo Wawi Chake Chake. 


Akifungua Kongamano hilo  Kwa niaba  ya Mrajisi wa  Asasi za Kiraia  Pemba Sada Abuu - Bakar  Muhammed Amewataka Vijana  kutumia vyema nafasi ya kushiriki   kuleta Maendeleo  ya nchi. 

Amesema endapo Vijana wataweza kushirikiana  ina kuzitumia vyema fursa zinazopatikana katika Nyanja Mbali mbal Bila kujali tofauti zao za Dini,  Rangi Mahala wanapotoka, imani itikadi, Pamoja na  siasa zao kutapelekea kupatikana Maemdeleo yao na Taifa. 


 Wakizungumza katika kongamano hilo la Majadiliano Baadhi ya vijana  Akiwemo  Nassir Juma, Pamoja na Zuleikha Maulid Heri wameiomba Serikali  Na Taasisi za Vijana Kusimamia  Vyema Masuala ya Sera na Mikakati  Inayoanzishwa  ili iweze kuwa endelevu  kwa Maslahi  ya Muda mrefu Kwa Vijana  na iondokane na kubadilika badilika. 

 Akizungumzia kongamano hilo    Suleiman Muyuni  kutoka  Kijana High Faundation  amesema Lengo la kongamano hilo ni kuwakutanisha vijana wa kada   za aina mbali mbali kuzungumza mambo yanayaowahusu vijana ili kusaidia kushiriki na  kutoa Mapendekezo ya kisera, mikakati na sheria  kwa Serikali zote mbili  ambazo zitasaidia kujenga Tanzania . 


Kongamano hilo lililokuwa na Lengo la kuhamasisha ushiriki na ushirikishwaji wa vijana katika masuala ya Maendeleo  hayo  Jumla ya Mada Tatu zinazohusu fursa, Maendeleo,  chamagamoto na Ushiriki wa vijana  ziliwasilishwa na  kutolewa Mapendekezo na Washiriki wa Mafunzo hayo.

Mwisho.

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI