MKURUGENZI PEGAO AELEZA MAFANIKIO YALIOFIKIWA KUTATUA KERO ZINAZOREJESHA NYUMA WANAWAKE KUFIKIA MAENDELEO YA KUWA VIONGOZI, ASISITIZA MASHIRIKIANO VIONGOZI WA SHEHIA KATIKA KUZIPATIA UFUMBUZI KERO HIZO.

NA AMINA AHMED MOH’D PEMBA. 
WAANDISHI wa Habari Wameaswa  Kutoa Taarifa ambazo zitasaidia kujenga uelewa kwa Jamii Juu ya  kupatiwa ufumbuzi  changamoto  zinazopelekea kutofikia Maendeleo  yao  kwa Wanawake ikiwa ni Pamoja na kupata Haki katika nafasi za Uongozi.

 Ametoa Ushauri huyo Mkurugenzi  wa Jumuiya ya PEGAO Kisiwani Pemba Hafidh Abdi Said,alipokuwa akizungumza na Waandishi  wa Habari katika Mkutano Maalum wa kutoa Taarifa kwa vyombo vya Habari juu ya  kazi zinazofanywa na   wahamasishaji jamii (Citizen Brigadi) katika wilaya uliofanyika katika ofisi za Jumuia hiyo Msingini Chake Chake Ikiwa ni utekelezaji wa Mradi  wa Kuwajegea Uwezo wanawake  katika Masuala ya Uongozi. 

Amesema  Wanawake na  wananchi wamekuwa wakikukabiliwa na changamoto mbali mbali, ikiwemo suala la Maji safi na salama, umeme kwa baadhi ya vijiji, Barabara, madaraja, elimu, vituo vya afya kufuata masafa marefu, changamoto ambazo zinaweza kutatua iwapo Waandishi wa Habari watatumia vyema kalamu zao kwa kushirikiana na Wahamasishaji hao , kuzisemea Changamoto hizo, kupatiwa ufumbuzi na kusaidia Kufikiwa Mlengo ya Uongozi kwa Wanawake . 

Katika hatua Nyengine Mkurugenzi Hafidhi alisema Mradi huo  kupitia Wahamasishaji jamii umefanikiwa kupatiwa ufumbuzi jumla ya  kero 17 katika kipindi kifupi cha uhamaishaji jamii, ambazo zilikuwa  zitaathiri zaidi wanawake kufikia lengo lao la kushiriki katika nafasi za uongozi ikiwemo kero za ukosefubwa huduma za Maji safi na salama. 

 Akizungumza katika Mkutano huo  Mratibu wa Tamwa Pemba Fat-hiya Mussa Said, alisema jamii imepata uwelewa wakutosha kutoka kwa wahamasishaji jamii, katika kuibua kero na kuweza kuzitatua, ambapo amewaasa Masheha na viongozi wa serikali kisiwani Peba  kushirikiana kwa pamoja kupitia kamati za shehia kwa lengo la kuandaa mikutano, ili kujadili changamoto zinazowakabilia wananchi na kuweza kupatiwa ufumbuzi.

Nae Mratibu wa PEGAO Dina Juma, alisema mradi huo utaendelea kufanikiwa  na kufikia Malengo endapo waandishi wa habari ni wataendelea kujikita katika kuandika na  kuhamaisha jamii, juu ya kushiriki katika nafasi za Uongozi na Demokrasia.

Mradi huo wa Mradi wa kuwajengea uwezo wanawake katika masuala ya uongozi unaendeshwa na TAMWA-Zanzibar, ZAFELA na PEGAO kwa ufadhili wa Ubalozi wa Norway ambapo  jumla ya kero 44 zimeubuliwa na wahamasishaji jamii katika Wilaya  zote kisiwani Pemba. 
MWISHO. 


Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI