WADAU WA KUPAMBANA NA UDHALILISHAJI WA KIJINSIA KWA WANAWAKE NA WATOTO WALIA NA SHERIA NAMBA 7 YA MWAKA 2018 , SHERIA YA MWENENDO WA MAKOSA YA JINAI, WAOMBA KUFANYIWA MABORESHO BAADHI YA VIFUNGU VYAKE.
NA AMINA AHMED MOH’D - PEMBA
"USIPOZIBA Ufa Utajenga Ukuta " Ni Msemo Ambao Mara Nyingi unapotumika Huashiria kuwepo kwa Dosari ya Jambo Fulani ambalo waliowengi Wameshindwa kuona Dosari hiyo na Dosari hiyo isipodhibitiwa Mapema huenda Kikaleta Madhara Makubwa Baadae.
Dosari ambayo inaendelea Kuumiza Vichwa vya Wadau na Wanaharakati wa Kupambana na Udhalilishaji wa Kijinsia ni Mapungufu ya Kisheria katika Baadhi ya Sheria ambazo zinatumika kupambana na Udhalilishaji.
Vifungu mbali mbali vya Sheria hizo Zanzibar ambazo huenda ikawa ni Moja kati ya Visababishi vinavyoendelea Kurudisha Nyuma Mapambano Dhidi ya kumaliza Vitendo Vya Udhalilishaji na kutoa Mwanya kwa wale ambao hutenda Makosa haya bila Aibu kuzidisha kasi.
Upelelezi wa kesi za Udhalilishaji Haujawekewa Muda Maalum wa kukamilika Upelelezi wake, Utolewaji Hukumu tofauti kwa Watuhumiwa ambao wamefanya Makosa yenye kufanana, Kuwepo kwa Hukumu Ndogo ambayo imewekwa kwa Mujibu wa Sheria kwa wanaotiwa Hatiani, Vifungu ambavyo vimetoa hukumu Kubwa Kwa Wanaotiwa Hatiani juu ya Makosa haya bila Waathirika wanaofanyiwa Vitendo hivyo kufaidika na Chochote Juu ya Hukumu Hizo zilizowekwa na Sheria.
NI IPI SHERIA HIYO INAYOUMIZA AKILI ZA WANAHARAKATI WA KUPAMBANA NA UDHALILISHAJI!
Moja kati ya Sheria ambayo imebeba vifungu vya Kusimamia Masuala ya Udhalilishaji ni Sheria Namba ( 7 ) ya Mwaka 2018 Sheria Ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai. Ambayo baadhi ya vipengele Vimekuwa Vikirudisha nyuma Mapambano hayo.
Kifungu cha 7 cha Sheria Namba 7 Mwaka 2018 kimeweka Mamlaka Kwa Mahakama ya Mkoa kutoa Adhabu ya kifungo Kisichozidi Miaka 14 na Faini Isiyozidi Milioni 14" .
Kifungu cha Adhabu kwa Makosa ya Udhalilishaji, Ulawiti, Kuingilia Kinyume na Maumbile, Kubaka kifungu 109 kifungu kidogo cha 1 kimesema kuwa "Adhabu kwa Kosa la Kubaka Ni kifungo Cha Maisha au Katika Mazingira Mengine yeyote, Adhabu isipungue Miaka 30".
Hata hivyo Sheria ipo Kimya juu ya kuchukuliwa Hatua za kisheria kwa Waathirika na Familia za Waathiriwa wa Makosa ya Udhalilishaji wanaokataa kutoa ushirikiano kwenye kesi .
Sheria hii ipo Kimya Juu kucheleweshwa kupewa Mwenendo wa Kesi kwa kesi ambazo wakili wa Serikali amekata Rufaa.
Moja kati ya Maswali Ambayo yanaendelea kukosa Majibu katika Vichwa vya Wananchi waliowengi ni Suala hili la Kutolewa hukumu Tofauti kwa wale ambao Mahakama imewatia Hatiani kwa Makosa yanayofanana.
Kukosekana kwa Usawa katika Utolewaji wa Hukumu katika Kesi za Udhalilishaji umekuwa sio Jambo Geni katika Masikio ya Waliowengi Unguja na Pemba .
Vyombo vya Habari Vimekuwa Vikitoa Siku hadi Siku Kesi Mbali mbali zenye Mfanano na Kosa sawa Lakini Hukosekana Mfanano katika Hukumu zake Zinapotolewa na Mahakama.
"Mfano Kesi za Ubakaji, Watenda Kosa Wawili Ambao wamehukumiwa katika Mahakama Tofauti Huripotiwa katika Mahakama Za Mkoa Unguja Na Pemba huripotiwa wakiwa wameshatolewa Hukumu tofauti huku wapo ambao huhukumiwa kutumikia Chuo Cha Mafunzo Kwa Kipindi kifupi, na wapo ambao hutumikia kwa kipindi Kirefu la kushangaza wakiwa na Kesi zenye Kufanana.
WANANCHI PAMOJA NA WANAHARAKATI WANA MITAZAMO GANI JUU YA SUALA HILI!
" Jamii Imekosa Hofu Juu ya Hukumu zinazotolewa na Mahakama zetu Leo Unasikia Fulani Kabaka Mtoto wa Miaka 11 Kafungwa Miaka 14 na Faini halipi Mwengine Kalawiti Mtoto kafungwa Miaka 7 na Faini halipi Sababu hatujui lakini Akili zetu zinaamini ni Rushwa kwa vile Makosa yamefanyika yapo sawa Alisema Abuu Bakar Zubeir Ali Mkaazi wa Chanjaani Chake Chake.
"Binafsi mimi Mpaka leo sijajua Hatma ya Mtoto Wangu wa Miaka 9 Ambae Alibakwa Mahakama ikamtia Hatiani Mtuhumiwa na Ikaamuru atumikie Chuo Cha Mafunzo Miaka 14 na faini shilingi Milioni 2 Lakini Mpka Leo hii Mtuhumiwa Yupo chuo Cha Mafunzo lakini bado faini hatujaipata ni kama ilitajwa tu kule Mahakamani. ".
" Nilijaribu Kufuatailia juu ya fidia hiyo lakini nilitakiwa nifungue kesi Mpya ya Madai, Naamini yasingekuwa hayo kama kungekuwa na sheria ambayo ingeweka ulazima wa Kulipa hizi fidia baada ya Mahakama kutoa Hukumu.
Alisema Baba Mzazi wa Mtoto aliefanyiwa Udhalilishaji Madungu Chake Chake ambae Jina linahifadhiwa.
" Kesi zinaripotiwa Nyingi Wananchi Wameamka sana kuyaripoti haya Matukio yanapojitokeza Masuali yamebaki mbona hakuna Mabadiliko kutokana hukumu zinazotolewa Bado yanendelea kujitokeza , Kama hofu imeondoka juu ya baadhi ya watu na kufanya Matendo haya ya kikatili huku sheria zikikaa kimya au zikiwa zinakinzana hatutofika Popote Kupambana na Udhalilishaji Serikali na Wadau waangalie kasoro iko wapi kwenye hili.
"Sina Uzoefu katika Mambo ya Sheria lakini Uzoefu wa kusikia haya Matukio kuripotiwa Kwa Adhabu tofauti ninao, nishasikia zaidi ya Mara Moja Mbakaji Wete kagungwa Miaka 30 Chake Chake Chake Miaka 14 Kama tatizo ni ukinzani wa Sheria Tunaiomba Serikali Iliangalie Suala hili. Alisema Abeda Ali Seif .
" Haiwezekani Kabisa Na ni udhaifu Mkubwa alietenda kosa Wete Na Alietenda kosa Chake hilo hilo wakahukumiwa Tifauti hapo kuna dosari kama sio ya Kisheria bhasi huenda kuna Tumika Rushwa kwa mtazamo wangu ni jambo la Aibu kiukweli.
" Sisi Kama wadau wa Kupambana na kupinga Vitendo vya udhalilishaji Tunatamani kuona Mabadiko ya Haraka Na kuwepo Na Sheria Moja tu ambayo itasimamia masuala haya ya Udhalilishaji Utitiri wa Sheria Tumebaini kuwa ni Changamoto inayorudisha nyuma Mapambano haya kwa sababu kila Mahakama inatoa.
Hukumu kwa kufuata sheria Yake kungekuwa na Sheria Moja juu ya Maswala haya naamini kusingekuwa na hizo adhabu tofauti kwa watenda Kosa wa aina Moja". Ni Maneno ya Fat hiya Mussa Said Mratibu wa Chama cha Waandishi wa Habari wanawake Zanzibar Ofisi ya Pemba.
" Tunajitahidi kwa Nguvu zetu Zote Kupambana na Udhalilishaji Tukiwa kama Wanaharakati ambao Tunaguswa Moja kwa Moja juu ya Suala hiliDosari Ni nyingi zilizomo katika Sheria si hiyo tu Ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai na Hata nyengine ambazo zinazasimamia Udhalilishaji zina Mapungufu".
"Niseme suala hilo la kuwepo kwa sheria nyingi Ambazo zinasimamia Vifungu vinakinzana ni Dosari Kuna haja ya kusimamia hili kuona kuna patikana Sheria Moja Tu ya Udhalilishaji. Tatu Abdalla Msellem Mwanaharakati Wa kupambana na Udhalilishaji kutoka Jumuia ya Tumaini Jipya Pemba.
Hassan Hamza Msellem ambae ni Mwandishi wa habari za Jinsia anasema kuwa "Tumekuwa Tukipokea lawama nyingi Tunapomaliza kutangaza Taarifa zetu , Jamii imekuwa ikitulaumu Wanasema mbona Fulani kapata Miaka Mingi, mbona Huyu Hachukuliwi Hatua Yule kapewa Miaka kidogo kana kwamba sisi ndio tuliotoa Maamuzi.
" Wapo kabisa ambao Wanahisi Mahakama hazitendi Haki juu ya Kesi hizi, Wengine kupata Hukumu Ndogo, Wengine kubwa Kesi zenye Kufanana Wanaona kama Rushwa ndio imetumika kuwe na ulazima wa serikali kukaa na Wadau na Wanasheria kuangalia hizi Geps kuona zinarekebishwa.
JEE ! NINI HUSABABISHA UTOFAUTI HUU WA UTOLEWAJI WA HUKUMU ?.
"Mahakimu kuwa na Mamlska Kisheria kutokana kuwepo kwa Baadhi ya Vifungu ambavyo Vinatoa Mwanya wa Hukumu Ndogo ambayo imewekewa Ukomo na vile Ambavyo Vimetoa Hukumu kubwa Ambayo haijawekewa Ukomo Endapo Mtu atatiwa hatiani na Mahakama juu ya Makosa yote ya udhalilishaji ikiwemo Ubakaji".
Ukizani wa Vifungu hivi vya Sheria Umempa Mamlaka Hakimu yeyote wa Mahaka za Mkoa kutumia Moja kati ya vifungu hivi Wakati Wanapofanya Maamuzi ya kutoa Hukumu kwa wanaotiwa Hatiani Jambo ambalo hupelekea kukosekana kwa Hukumu sawa kwa Watendaji wa Makosa yanayofanana.
Licha ya Mamlaka hayo Lakini pia Vifungu vya Adhabu ndani ya Sheria hiyo Pia vimeonesha Ukinzani Juu ya Mamlaka hayo kutokana na Adhabu Kubwa ambazo Zimekuwa na Ugumu kutekelezwa kwa Mujibu wa Sheria na kupelekea Kesi za Udhalilishaji kuendelea kuripotiwa Siku hadi Siku bila watendaji wa Makosa hayo Kuingiwa Hofu Alidai Ali Amour Makame Wakili wa Serikali kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Pemba.
Kuna Mahakimu Wengine wa Mahakama Ya Mkoa (Wanafunga) Wanapeleka Chuo Cha Mafunzo Miaka 30 , Lakini kuna Wengine Wanapeleka Chuo Cha Mafunzo (Wanafunga) Miaka 14 ni kutokana na Kufuata Sheria hii ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai kuwa imetoa Uhuru kwa Mahakimu Wa Mahakama za Mkoa Kufuata Vifungu hivi Ambavyo vimewapa Mamlaka kisheria Alifafanua Mwanasheria Huyo.
NI YAPI MAONI YA WADAU JUU YA SHERIA HII ZAIDI KATIKA KUTOA ADHABU SAWA KWA WANAOTIWA HATIANI KUFANYA KOSA LA AINA MOJA.
"Mimi Maoni yangu Mahakama za Mkoa zitoe adhabu sawa ikiwa Alietenda kosa la Ubakaji atapata adhabu ya Kifungo cha Miaka 30 na Faini bhasi iwe hivyo kwa wote Mahala Popote ili kusiwe na ukizani wala Tofauti Alishauri Ali Amour Makame.
Bora Mahakama zote wafuate kifungu Cha Adhabu ambacho kimetoza adhabu kuwa Watuhumiwa wote wa Makosa hayo ya jinai wafungwe Miaka 30 wasitofautiane Aliongeza.
" Serikali Iweke Sheria ambayo Itaweka ulazima wa kulipwa izi Fidia Ili waathirika wa matendo haya wapate fidia Kwa sababu zinaishia kusemwa tu hazitolewi Jambo ambalo halieti Tija yeyote zaidi ya Maumivu ya Kwa Waathirika na hii itawezekana Endapo Kutakuwa na Sheria Moja ya Udhalilishaji ambayo Itaangalia yote haya na kurekebishwa. Fat hiya Mussa Said.
Waandishi Wa Habari Wanamchango Mkubwa juu ya Hili Watusaidie kuoneshana kusemea hizo Dosari ambazo kwa sasa zinaonekana ni ndio lakini Madhara yake ni makubwa na Niendelevu ili kupatikane Marekebisho.
kwa Kiasi kikubwa Vifungu vya Sheria hii Vinawapa Nafasi Wanaofanya Makosa kupata Mwanya Wakuendeleza Makosa yao na ndio maana hayamaliziki katika Jamii Sheria Bado Hazijawabana, Endapo Maboresho katika Sheria hii na nyengine zitaondolewa zile Dosari ambazo zimetoa Mwanya na kupatikana Sheria Moja Madhubuti itakayosimamia Udhalilishaji huenda Vitendo hivyo vikapungua na Kumalizika Kabisa.
Mwisho
Comments
Post a Comment