Posts

Showing posts from March, 2025

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.

Image
 NA ASIA MWALIM  MARA nyingi tumeshuhudia uzinduzi wa mipango mikakati kwenye masuala mbali mbali ikizinduliwa,  lakini ukifatilia kwa karibu utabaini utekelezaji wake haufikii lengo husika.   Kwa kuwa utekelezaji wake hauzingatiwi, huo huwa wakati kwa baadhi ya watu kutokujali kutekeleza yalioelezwa kutokana kutochukuliwa hatua yoyote.   “Huwezi kumwambia mgeni apite wakati mlango wa nyumba yako umeufunga” huu ni wakati sasa serikali, wadau mbali mbali wa michezo na jamii kushirikiana katika utekelezaji wa mpango mkatati jumuishi wa michezo ili kufikia dhana ya kuanzishwa kwake na kila mmoja kunufaika na fursa za michezo.   Kwa muda mrefu kundi kubwa la wanawake na wasichana walishindwa kushiriki michezo ipasavyo kutokana na changamoto kadhaa ambazo hazina usalama kwao kushiriki michezo.   Hali hiyo ni miongoni mwa vikwazo vinavyowakabili baadhi ya wanawake wanaojitokeza kushiriki michezo, hatimae kuvunja ndoto zao ya kuibua vipaji kwa kut...

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Image
NA AMINA AHMED PEMBA. WANANCHI katika  Manispaa ya Mji wa chake chake na Vitongoji vyake walilazimika kuchelewa kakika harakati zao za kujitaftia riziki baada ya usafiri uliozoeleka kwa siku za hivi karibuni wa Bajajj kutoonekana au kuonekana chache kwenye viunga tofauti mapema leo Machi, 6, 2025. Baada ya hali hiyo kushika kasi huku wananchi wakipigwa na butwaa, mnamo Majira ya saa 3 Asubuhi  Gari za Daladala ikiwemo za Ole Kianga kuanza kuchukua Abiria hao na kuanza kuwasafirisha. Hata hivyo wakizumzia kutoonekana katika vijiwe vyao kubeba abiria baadhi ya waendesha Balaji walisema kuwa walilazimika kushiriki katika kikao  cha  dharura  kwa ajili ya kujadili  unyanyasaji wanaopata katika mamlaka za serikali ikiwemo Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi kupitia mamlaka ya usafirishaji. Wamesema Mawasiliano na Baraza  MawasilianoJuu kile walichodai kuwa Wamechoshwa na Udhalilishaji wanaofanyiwa na Mamlaka hizo mb...