Posts

Showing posts from June, 2024

150 KUSHIRIKI RIADHA WAKIWEMO WANAFUNZI KUADHIMISHA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA TAREHE 29 MWEZI HUU

Siku ya Mtoto wa Afrika Zanzibar CHAMA cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ) kwa kushirikiana na Idara ya Michezo, Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA), Taasisi ya Maendeleo ya Mashirikiano ya Ujerumani (GIZ) na Kituo cha Mijadala kwa Vijana (CYD), inatarajia kuadhimisha ya siku ya kimataifa ya Mtoto wa Afrika tarehe 29 Juni 2024 kwa kuandaa mashindano ya riadha kwa wanafunzi wa skuli mbalimbali za Zanzibar. Maadhimisho hayo yatawahusisha jumla ya washiriki 150 ambapo kati ya hao watakaoshiriki mashindano ni wanafunzi 75 kutoka katika skuli za Unguja ambazo zimeshajiandaa kushiriki mashindano hayo. Tukio hili muhimu ambalo linalenga kuhamasisha usawa wa kijinsia katika michezo litawaleta pamoja wadau kutoka taasisi za kierikali na zisizokuwa za kiserikali ikiwemo wanafunzi kutoka skuli mbalimbali za Unguja, wanamichezo, walimu wa michezo, na wadau wote wa masuala ya usawa wa kijinsia. Maadhimisho haya yanatoa fursa kwa wasichana kuone...

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

Na Amina Ahmed Muhamed Pemba. WAZAZI na walezi  wameatakiwa kufuatilia kwa ukaribu nyenendo  na tabia za watoto  pamoja na  vijana  wao  ili kuwanusuru kujiingiza katika tabia hatarishi za kutumia madawa ya kulevya  . Kauli hiyo imetolewa na  waziri wa nchi ofisi ya makamu wa kwanza wa rais zanzibar Harus Said Suleiman katika ufunguzi wa kongamano  la maadhimisho ya siku ya kupiga vita  matumizi  na  usafirishaji wa dawa za kulevya duniani lililoanadaliwa  na mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya zanzibar katika  ukumbi wa makonyo wawi chake chake mapema leo. Amesema  bado kuna changamoto kubwa katika malezi na usimamizi wa watoto hususan ni kundi la vijana  jambo ambalo  linapelekea kuwa na idadi kubwa ya  vijana wanaotumia madawa ya kulevya na kupelekea kuharibu  maisha yao kwa kujiingiza katika vitendo viovu ikiwemo wizi .   "Bado kuna tatizo katika kusimamia malezi husu...